Zifuatazo ni sifa 15 za Mjasiriamali.
1. Ubunifu
Ubunifu ni kionjo cha muhimu sana katika
Ujasiriamali.Kwa kwawaida mjasiriamali anapenda kuwa tofauti ili awashangaze
watu.Anapenda kuwa mwanzilishi wa vitu au jambo.
2. Uwezo wa
kubaini fursa katika Matatizo
Vijana walioko ktk mazingira hatarishi au chokoraa mjini Arusha
walipokaa kikao kubuni mbinu ya kujikimu waligundua fursa ya kuosha vioo vya
magari pale mianzini kwenye mataa (Trafic lights) na kwa kufanya hivyo kwa
kujitolea wakawa wanapata fedha nyingi
kutoka kwa madreva
waliofurahi kuoshewa vioo vya magari yao tofauti na biashara yao ya awali
ya kuombaomba. Hivyo
hawa waliona tatizo la vioo vichafu
vya magari ikawa
ni fursa kwao ya kupatia
ajira.
3. Kujituma na kujitolea
Fursa nyingi za kijasiriamali zilipatikana
pale ambapo mtu alipoamua kujitolea
na kujituma bure bila malipo yoyote; hii ni sifa ya Muhimu sana kwa
mjasiriamali yeyote. .
4. Kuhitaji mafanikio
Mjasiriamali anaamini katika maendeleo na
akilini mwake anajua anachokifanya kitamtoa katika hali aliyo nayo. Mara nyingi
huyu mjasiriamali anapenda kuendelea
kuwepo katika ramani
ya mafanikio; hivyo njozi
yake, wimbo wake na maneno yake ni mafanikio.
5. Kuvumilia changamoto
Mjasiriamali kwa kawaida anakumbana na
changamoto zinazotishia uchumi, familia na hata heshima yake pale anapoanza
kufanya jambo au mradi. Hii ni sifa ya ujasiri ambayo inabeba neno ujasiriamali.
.
6. Uhuru
Uhuru ni kionjo kingine cha mjasiriamali
kwani anaamini kuwa akifanya mambo yake bila kuingiliwa na mtu mwingine anaweza
kufanikisha kile anachokikusudia. Mjasiriamali anapenda kufanya kazi yake
anavyoona yeye kupitia katika mazingira yake na raslimali zinazopatikana katika
mazingira husika. Daudi ni mfano wa mjasiriamali ambaye alikusudia kumuua
Goliati na walipojitokeza ndugu zake pamoja na mfalme wakimpatia mbinu zao za
kumshinda Goliati; Daudi alichagua kuziacha mbinu zao akaona mbinu yake
aliyoitumia siku zote porini kuulia dubu na samba waliokuwa wanamwibia mifugo
ingelimfaa kumuulia Goliati; alitumia mawe matano, kombeo na fimbo kumkabili na
kumuua Goliati(I Samwel 17:1-58).
7. Kudhubutu kwa Angalizo.
Mjasiriamali ni mtu ambaye anaanzisha mambo na
kuyasimamia na kuyasimamia mpaka atimize lengo lake bila kukata tamaa;
vilevile ni mtu anayejua kuwa kukosea
anapata darasa la kujifunza na katika kutenda kuna mafanikio. Mjasiriamali mmoja
asiyejulikana aliandika maneno haya kwenye mtandao wa jamii kuwa “ If FAIL
you never give up because F.A.I.L
means “First Attempt In Learning” END is not end. In fact, E.N.D means “Effort
Never Dies”. If you get NO as an answer , remember N.O means
“ Next opportunity”(Kama utashindwa
usikate tamaa kwa sababu kushindwa inamaanisha Jaribio
la kwanza katika kujifunza; Mwisho siyo mwisho ila ni kusema kweli Mwisho
maaana yake Bidii haipotei na
kama utapewa jibu la hapana kumbuka kuwa Hapana
maana yake ni Fursa ya Pili.
Kuwa mjasiriamali siyo
kufanya mambo bila
tahadhari ila ni kudhubutu katika mchakato wa kubadili maneno kuwa kitu
au kuingiza maneno katika matendo.
8. Kumiliki
Kumiliki kitu ni sifa ya ujasiriamali hata kama ni kidogo; ndiyo maana
mjasiriamali yupo tayari kumiliki huduma au biashara anayoifanya hata kama ni
kidogo mpaka iwe taasisi kubwa au kampuni kubwa. Nabothi ni mfano mzuri wa Mjasiriamali aliyekataa kuuza hati
miliki ya biashara yake aliposema kuwa “. .
. Bwana apishe mbali nikupe wewe urithi wa baba zangu”(IWafalme 21:3).
9. Kuona mbali
Mjasiriamali anao uwezo wa kuhisi jambo
linalokuja na jinsi ya kuweza kulikabili; hivyo huyu mtu anao uwezo wa kuona
mbali maili nyingi zaidi
ya wengine na hata anao uwezo wa kuelewa njozi
ambazo mwingine amekosa tafsiri yake. Kutokana na uwezo wake wa kuona
mbali anao uwezo wa kupata utatuzi wa shida au jambo kwa haraka zaidi ya watu
wengine. Mfano mzuri wa Mjasiriamali kuona mbali kuliko wengine ni Yusufu aliyetafsiri ndoto ya mfalme akajikuta
ameokoa Misri na kipindi cha njaa cha miaka Saba iliyokuwa mbele yao mpaka na
ndugu zake Waisraeli (Wana wa Yakobo) wakaja kuponea Misri. (Mwanzo 41:14-57)
Mjasiriamali anao uwezo wa kutatua tatizo kwa
kulifanya kuwa faida, mradi au biashara kwake na kwa jamii inayomzunguka.Hivyo
anakuwa ametatua tatitizo kiubunifu. Miaka ya 2006 kuelekea 2010 nilikuwa
naishi katika mji wa Arusha maeneo ya Big Y lakini ofisi zangu za kazi zilikuwa
Njiro, Kijenge, na Ungaltd; Kilichonikera sana ni kuwahi ofisini asubuhi kwani
mara nyingi nilikuwa natembea kwa miguu katika barabara Big Y na ile ya Philips
kwenda Impala na nikagundua kuwa watu wengi nao walikuwa wanatembea kwa miguu; ndipo nilipoona kuwa kama nitakuwa
natumia pikipiki ya baba mmoja aitwae Anton kunibeba nitakuwa
nawahi na ndipo nilipokubaliana na rafiki yangu kuweka pikipiki za bodaboda
katika keepleft ya impala na tulipata wateja wengi sana kwani tulitatua tatizo
la kutembea kwa migiuu kiubunifu na huo ukawa mwanzo wa kutumia bodaboda
katika mji wa Arusha.
11. Uwezo wa kujiliana.
Mjasiriamali mmoja aliandika akisema
hivi “A Matter
of Pespective: Most problems won’t exist if people understood the
difference between argument and discussion. Argument =Finding
out who
is right. Discussion=Finding out what is
right. (Ni swala la mtazamo: Matatizo mengi yasingekuwepo Kama watu wangefahamu tofauti kati ya kushindana na kujadiliana. Kushindana=Ni kutafuta
ninani sahihi. Kujadiliana = Ni kutafuta
ni
kipi sahihi.) Mjasiriamali ni mtaalamu
wa kufanya majadiliano ili kujua kitu sahihi ili aweze kufanikisha ubunifu
wake; Na kwa kuwa na uwezo wa kujadiliana inamwezesha mjasiriamali kufanikiwa
katika huduma au biashara yake kwani mahusiano yanadumishwa kati ya mtoa
huduma(Mjasiriamali) na wapokea huduma au wateja.
12. Uwezo wa kuamua jambo katika hali hatarishi
Katika hali hatarishi
ndiyo mazingira mazuri
ya mjasiriamali anaamua mambo yake tofauti na wengine; Kwani
mjasiriamali kwake ni furaha
kupambana na changamoto zinazochanganya au kuogopesha wengine wengi. Hii ni sifa juu sana ya mjasiriamali ambayo ni Ujasiri katika kuamua na kutenda. Mtaalamu mmoja aliwahi kusema kuwa ni "afadhali kigugumizi cha kuongea kuliko kigugumizi cha kufanya maamuzi."
13. Uwezo wa kuongoza.
Mjasiriamali ni kama dreva ambaye anayo sifa
ya kuendesha na huduma au biashara yake kuanzia mwanzo hadi pale atakaposhuhudia ikifanikiwa. Kazi kubwa
ya mjasiriamali ni kuonyesha namna ya kufanikisha njozi zake na kusimamia kile
ambacho moyoni anajua kuwa kitamfanikisha yeye na jamii
inayomzunguka;Ni kwa nadra
sana mjasiriamali atasimama au kukaa na kuagiza akitoa amri juu ya amri
kama kiongozi yeye mara nyingi atasimama nafasi ya mwelekezaji au mwongozaji wa njia ya kufanikisha
kusudi la Bisashara au huduma husika.
14. Uwezo wa Kutetea jambo.
Professa wangu wa kozi ya Uandishi wa
Andiko Utafiti (Research Paper) tukiwa darasani aliwahi kutuambia kuwa kama
utaandika andiko lako unatakiwa uwe tayari kutetea kile ulichoandika kwani ni sawa na mtoto wako;Hawezi mtu hata kama
ni mwalimu wako ni vizuri ujue jinsi ya kutetea andiko lako; Ndiyo maana Katika
shahada zote kuanzia ule ya uzamili na kuendelea kuna wakati wa kutetea Andiko utafiti
(Defence of Research
Paper) na hili linafanyika ili kuweza
kueleza maana ya kile ulichofanyia utafiti.
Hivi ndivyo ilivyo kwa mjasiriamali yeyote
anatakiwa awe tayari kutetea kuhusu mradi
wake ili hata
kama baadaye iwezekane kusaidiwa na taasisi rasmi na sisizorasmi za kifedha.
15. Kujiamini.
ya kujiamini kama mjasiriamali.
Asante sana pastor kwa ujumbe mzuri
JibuFuta