SOKA IGIN

WE INSPIRE AND EMPOWER FOR CHRIST'S MISSION.

Alhamisi, 29 Machi 2018

TOFAUTI 7 KATI YA MFANYABIASHARA NA MJASIRIAMALI


Zifuatazo ni tofauti Saba kati ya Mfanyabiashara na Mjasiriamali


Mfanyabishara anaogopa mabadiliko wakati Mjasiriamali anafurahia Mabadiliko

Mfanyabishara hana dira wala mwelekeo wa biashara yake lakini
Mjasiriamali anao mwelekeo wa bishara yake.

Mfanyabiashara hajitumi na hugusa hiki na kile bila   kukikamilisha
wakati Mjasiriamali hujituma na kutumia nguvu na mali katika jambo moja
.
Mfanyabiashara si mbunifu na ni tegemezi; anaiga wengine    lakini
Mjasiriamali ni mbunifu na mwenye kujitegemea .

Mfanyabiashara anafanya kazi zake kwa mashaka hana uhakika na maisha ya baadaye ila Mjasiriamali anafanya kazi kwa matumaini ya siku za baadaye.

Mfanyabiasha  ni  Mwoga  kufanya  maamuzi  wakati Mjasiriamali
haogopi kufanya maamuzi.

Mfanyabiashara hana akili ya kujifunza; yeye anapendelea kuiga wengine na hana mtandao wa biashara wakati Mjasiriamali anayo akili ya kujifunza na anao mtandao wa biashara.
(Chiraka Muhura, Ujasiriamali Kwa Maisha Bora,(Dar-es-Salaam :Hope Publishers, 2014) 22)


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni