SOKA IGIN

WE INSPIRE AND EMPOWER FOR CHRIST'S MISSION.

Alhamisi, 29 Machi 2018

MAMBO 7 YA MSINGI YANAYOHITAJIKA KATIKA MAOMBEZI


Kitabu cha Danieli Sura ya Tisa kinatoa mfano elekezi wa Maombezi . Katika Ombi hili la Danieli tunapata sifa za mwombaji au sifa za ombi lenyewe kama ifuatavyo.

      i.       Mwombaji anakubaliane na Neno la Mungu
Katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danieli kwa kuvisoma vitabu nilifahamu hesabu ya miaka  ambayo neno la Bwana lilimjia  Yeremia nabii . . . .” (Daniel 9:2)

     ii.       Mwombaji  aonyeshe uzalendo
“Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga  na kuvaa nguo za magunia na majivu”(Daniel 9:3)

   iii.       Mwombaji ajikane nafsi
Nikamwomba Bwana, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mwenye kutisha ashikaye maagano na rehema kwao wampendao na kuzishika amri zake” (Daniel 9:4)

   iv.       Mwombaji asijitenge na watu wa Mungu
“Tumefanya dhambi, tumefanya ukaidi, tumetenda maovu, tumeasi, naam, hata kwa kuyaacha maagizo yako na  hukumu zako.” (Danieli 9: 5)

     v.       Mwombaji aimarishwe na Toba
“Tumefanya dhambi, tumefanya ukaidi, tumetenda maovu, tumeasi, naam, hata kwa kuyaacha maagizo yako na  hukumu zako .  .  .  wala hatukusikiliza watumishi wako,manabii ambao kwa jina lako walisema na Wafalme wetu . . . Ee Bwana haki ina wewe, lakini kwetu sisi kuna haya ya uso kama hivi leo . . . Rehema na msamaha ni kwa Bwana Mungu wetu, ingawa tumemwasi. . . Na sasa , Ee Bwana Mungu wetu uliyewatoa watu wako hawa katika nchi ya Misri kwa mkono hodari, ukajipatia sifa, kama, kama ilivyo leo; tumefanya dhambi, tumetenda maovu “(Danieli 9: 5-15)

   vi.        Mwombaji aitegemee tabia ya Mungu
 Nikamwomba Bwana, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mwenye kutisha ashikaye maagano na rehema kwao wampendao na kuzishika amri zake. Ee Bwana haki ina wewe  lakini kwetu sisi kuna haya ya uso . . . Rehema na msamaha ni kwa Bwana Mungu wetu ingawa tumemwasi. Na sasa , Ee Bwana Mungu wetu uliyewatoa watu wako hawa katika nchi ya Misri kwa mkono hodari, ukajipatia sifa, kama, kama ilivyo leo; tumefanya dhambi, tumetenda maovu “(Danieli 9:4, 7, 9, 15)

  vii.       Mwombaji awe na lengo la kumpatia Mungu utukufu
“Ee Bwana sawasawa na haki yako yote nakusihi hasira yako na ghadhabu yako zigeuzwe na kuuacha  mji wako Yerusalemu, mlima wako mtakatifu, maana kwa sababu ya dhambi zetu na maovu yetu  ya baba zetu . . .  Ee Mungu wangu tega sikio lako ukasikie fumbua macho yako ukautazame ukiwa wetu, na mji uke ulioitwa kwa jina lako; maana hatukutolei maombi yetu kwa sababu ya haki yetu, lakini kwa sababu ya rehema zako nyingi. . .  Ee Bwana, usamehe; Ee Bwana,usikilize, ukatende, usikawie; kwa ajili yako wewe Ee Mungu wangu; kwa sababu mji wako na watu wako wanaitwa kwa jina lako.” (Danieli 9:16-19)

Kwa kujifunza zaidi jipatie kitabu kiitwacho "MAOMBI NA MAOMBEZI" Wasiliana na 0788010398. 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni