SOKA IGIN

WE INSPIRE AND EMPOWER FOR CHRIST'S MISSION.

Jumatatu, 2 Aprili 2018

MBINU 10 ZA KUSAIDIA KUOMBA MAOMBI YA MLIMANI




Maombi ya mlimani ni maombi yenye kusudi maalumu yanayofanyika mlimani, porini,shambani, chumbani, pembeni mwa bahari,mto ziwa au eneo lolote ambalo kuna utulivu wa kutosha.[1] .

 Nyakati zote za safari ya kanisa tangu Edeni, kanisa limepitia katika uzoefu wa maombi ya mlimani. Uzoefu huu wa maombi ya mlimani unathihirika wazi wazi katika kitabu cha Matendo. 

Maombi ya mlimani ilikuwa ni moja ya kanuni aliyoitumia Mtume Paulo katika kuotesha na kuliongoza kanisa katika kipindi kigumu cha kanisa la mitume. 

Lyrene akiandika katika kitabu chake cha “Prayer and Evangelism” anasema kuwa “Kanuni ya Maombi ya pamoja, au maombi ya kusudi na nia moja, ni mkanda unaofunga kitabu kizima cha Matendo ya Mitume. Maelezo ya awali ya Daktari Luka kuhusu  wale 120 (Mdo.1:15) yanaonyesha kufuatwa na agizo la Kristo la kumsubiri Roho Mtakatifu kwa kutii na kuomba kwa nia moja kama kundi. Nguvu ya maombi ya pamoja inatambuliwa tena wakati Baraza la Sanhedrin walipotishia wafuasi wa Yesu kwa kuwakataza na kuwatisha kuwa wataadhibiwa kama wataendelea kuongea kuhusu “jina la Yesu”(Mdo.4:18).   Nia ya kuhubiri ilikuwa kubwa sana, hata hivyo, na mikutano ya maombi ya pamoja ilielekezwa kwa kanisa la awali kama daraja jipya la ujasiri (Mdo.4:31). “Wakiwa na ujasiri katika kushuhudia, walikuwa wote ni majasiri katika maombi."[2] Kama maombi haya yalivyohitajika kwa kanisa la awali; kwa sasa bado ni hitaji kubwa kwa kanisa la karne ya 21.

Zifuatazo ni mbinu 10 za kusaidia kuomba maombi ya mlimani

1.   Chagua Muda mzuri (Mhubiri 3:17)
2.   Chagua mahali pazuri penye utulivu (Marko 1: 35)
3.   Ikiwezekana siku hiyo iweni katika kufunga ( Mathayo 6:6-18)
4.   Shirikisha rafiki zako  (Mhubiri 4:9-10)
5.   Tumia mikao inayokupa uhuru na isiyochosha wakati wa maombi
6.     Kuwepo na muda wa sifa, shukrani na shuhuda za imani (Zaburi 50:15)
7.   Ikiwezekana tumia muziki uliotulia wa kumwabudu na kumsifu Mungu (2Nyakati 5:12-14)
8.   Epuka kuvunja taratibu za kidini na kijamii. (Warumi13:1)
9.   Kuwepo na Muda wa kusoma na kulitafakari neno la Mungu kwa wingi.
10.       Kuwepo na ratiba maalum ya tukio na ifuatwe.
-         Jina la kipindi na mhusika wa kipindi
-         Muda wa kipindi
-         Mambo ya kuombea
-         Muda wa mapumziko, kutafari binafsi


[1] Igin Soka, Kwanini Maombi ya Mlimani, Masomo ya maombi ya Wainjilisti walei -TPC Effort, 1997
[2]  Notable exceptions to this statement must be recognized. For a concise summary of the issue see E. C. Lyrene, Jr., "Prayer and Evangelism," Evangelism in the Twenty First Century (ed. by T. S. Rainer; Wheaton: Harold Shaw, 1989), 99.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni