Nabii Ibrahim ambaye ni rafiki wa Mwenyezi Mungu
anasimama kama baba yetu wa Imani zote na ndiyo maana jamii ya Wakristo na
Waislamu wanayo asili moja ambayo ndiyo iwafanyayo wasimame imara hata leo.
Lakini twaweza kujiuliza swali ieweje mimi mwislamu niwe na asili moja na mkristo kupitia
kwa Ibrahimu na tusifahamiane? Huo
undugu ulianza lini?;ndiyo maana hata Miriam (dada yake Musa) alipata ukoma kwa
kumsimanga Sipora(Mke waMusa) alipomhoji kaka yake kuwa umemwoa mwanamke mweusi
sana tena ambaye siyo uzao wa Ibrahim! Asijue kuwa naye Sipora alikuwa uzao wa
Ibrahimu Kupitia kwa mkewe wa tatu aliyeitwa Ketura (Mwafrika mweusi kutoka
Ethiopia)hivyo kwa hilo tu Mwenyezi Mungu akakasirika akampiga kwa ukoma(Hesabu
12:1-9);Na hili linajirudia katika karne yetu je wakristo na waislamu ni wote
ni wa Uzao wa Ibrahimu?
Sasa ni kwa vipi
tunakuwa uzao wa Ibrahimu? Undugu kati ya Mwislamu na Mkristo umetokea
mbali;
- Namna ya kwanza inahusu uzazi wa kimwili ambao ni wale wote waliozaliwa na Ibrahim kupitia kwa Hajiri ambao ni uzao wa Ishmaeli
- Namna ya pili niWaliozaliwa na Ibrahim kupitia kwa mkewe Sara ambao ni uzazi wa Isaka
- Mwisho ni Uzazi wa Imani ambao ni kwa wote wanaomwamini Masih Isa(Yesu);wote hawa wanahesabiwa kuwa wana wa Ibrahimu (Wagalatia3:29)
- Hata hivyo ndugu msomaji ni vizuri utambue kuwa Ibrahim hakuishia kwa mke wa pili bali katika uzee wake alimwoa mwanamke mwingine Mwarabu Mweusi(Mkushi) kutoka Ethiopia ambaye anamzaa Midiani na huyo Midiani anamzaa Yethro na Yethro anamzaa Sipora mke wa Musa.ambaye historia inasema yeye ni asili ya kabila nyingi za Waarabu (Mwa.25:1-6;1Nyak.1:32;Kut.18:10-11) American Tract Society Dictionary).
Nipende
kukujulisha kuwa changamoto kubwa ya kufahamiana ipo katika uzazi huu wa imani
na ndiyo maana Masih Isa katika kitabu
cha Injili anasema kuwa uzazi huu wa sisi kuwa wana wa Ibrahimu kwa imani si
uzazi wa damu wala mapenzi ya mwili wala mapenzi ya mtu bali kwa Mungu yaani
kwa lugha nyingine wote wanaomwamini Masih Isa(Yesu);wote hawa wanahesabiwa
kuwa wana wa Ibrahimu (Yonana1:13)
Inatia moyo
sana kwani koo hizi mbili upande wa Ishmael (Waislam) na
Ishaqa(Wakristo) tangu enzi za Nabii Ibrahimu wamekuwa na Umoja thabiti katika
matukio Muhimu ambayo hata kwa sasa twaweza kuendeleza katika wakati wetu ili
kuwaenzi wazee wetu na kumpatia mwenyezi Mungu utukufu.
- Wakati wa kifo cha Mzee Ibrahimu watoto wake wote walishirikana katika huduma ya mazishi; “Ibrahim akafariki, naye akafa katika uzee mwema . . . Isaka na Ishmaeli wanawe wakamzika katika pango ya Makpela, katika shamba la Efroni bin Sohari Mhiti,lielekealo Mamre .”(Mwanzo 25:8-9); Kwa wakati wetu kinachoshangaza kutokana na misimamo yetu ya Imani tofauti zinazopishana vitabu vya Mwenyezi Mungu tumediriki hata kutoshirikiana katika mambo ya msingi kama majanga ya Misiba njaa na magonjwa; hebu tufuate vitabu tuendeleze umoja wetu kati ya wakristo na waislamu tusimamishe Itikadi ya vitabu.Wakati Nabii Musa alipomuua Mmisri alikimbilia kwa Yethro mtoto wa Midiani na mjukuu wa Ibrahim kwa Ketura mke wake wa tatu;na akatunzwa huko na hawa Waarabu weusi mpaka Mzee Yethro alipompatia Sipora binti yake awe mkewe. (Kutoka 2:15 ;Mwanzo 25:1 – 2);Neno la Mungu linatupatia majina ya huu uzao wa Ibrahimu kwa Ketura kwa kusema “Na wana wa Ketura,suria yake Ibrahimu; yeye Zimrani, na Yokshani, na Medani, na Midiani na Ishbaki na Shua.Na wana wa Yokshani; Sheba na Dedani.Na wana wa Midiani;Efa, na Eferi na Hanoki, na Abida na Eldaa.Hao wote ndio wana wa Ketura(1Nyak.1:32-33); watoto hawa wa Ketura ni mababu wa zamani wa makabila mengi ya Kiarabu.( Keturah-American Tract Society Dictionary)
- Wakati Yesu(Masihi Isa) alipozaliwa tunaona Waislamu(Mamajusi wa mashariki) walikuja mpaka Bethlehemu ya Uyahudi wakiifuata nyota yake mashariki wakamsujudia na kumpatia dhahabu,Uvumba na manemane. ( (Mathayo 2:8- 11) Hawa walikuwa Waarabu (waislamu) ;Tunaona wachungaji wa kondoo Waebrania nao wanapewa ujumbe wa kuzaliwa kwa Yesu (Masihi Isa) na Mungu alitumia kundi la malaika kuwajulisha habari hiyo ya pekee(Luka 2:8-13). Mwenyezi Mungu alijua kuwa Waarabu(Waislamu) na Waebrania(Wakristo) ni watoto wake kupitia kwa baba mmoja kwa uzazi ila wenye tamaduni tofauti naye akapitia katika tamaduni hizo kuwajulisha habari hii kubwa ya kuzaliwa kwa Masihi Isa(Yesu); Kwa Waarabu Mamajusi alitumia ndoto na nyota ya mashariki kuwaonyesha Yesu alikozaliwa ila kwa Waebrania alitumia kauli ya malaika; kwani ilikuwa ni muhimu kwa watu wote kujulishwa kuzaliwa kwake kwa sababu siku ya kyama(yawm qyamat) atakayehukumu ni Masih Isa(Yesu) au mfalme wa Wafalme kwa kiarabu ni Malik-al-Amlak.(Al-Bhukhari Vol.8, Hadith 224,uk.16)
- Mtume Muhammad( SAW) pamoja na Marafiki zake wa karibu(Maswahaba) ilikuwa desturi yao kushirikiana na watu wa imani nyingine na huu ndio msimamo wa vitabu vya dini; wakati fulani tunaona akimkodishia Myahudi shamba lake lililokuwa Khaibar kwa mapatano ya kugawana mazao “ Inasimuliwa na ‘Abdullah’ Mtume wa Allah Alikodisha shamba lake lililoko Khaibar kwa Myahudi kwa masharti kuwa watalilima na kulitunza na watagawanya mazao yake nusu kwa nusu”(Sahih Al Bukhari Vol.3,Hadith # 678,Uk.409.
- Mtume Muhammad SAW akiwasisitiza Waislamu kufuata mafundisho ya wayahudi na Wakristo Inchi kwa Inchi ‘Abu Said Al Khudri amearifu kuwa mjumbe wa Allah (Amani iwe juu yake) alisema hivi Mwaweza kukanyaga katika njia ile ile ya mapito yaliyopitwa na hao inchi kwa inchi na hatua kwa hatua hasa,ili kwamba kama watatumbukia kwenye shimo lenye mjusi(guruguru), nanyi mfuatane nao humo pia.Tukasema:Mjumbe wa Allah,unamaanisha Wayahudi na Wakristo(Kwa maneno yako) wale wa kabila yenu? Akasema: Sasa ni nani mwingine zaidi ya makundi hayo ya dini? (Sahih Muslim Vol.8 Hadith # 6448 uk.39- Following the Footsteps of the Jews and the Christians)
- Mwisho kabisa tunaona hata swahaba wa Mtume Muhammad akitumia jengo la kanisa kuswalia kama inavyosimuliwa na Umar Said akisema “Hatuingii katika kanisa lenu sababu ya Sanamu na picha,Ibin Abbas amekuwa akiswali ndani ya kanisa alilopatiwa kwa sababu hapakuwa na sanamu ndani yake”(Sahih Al Bukhari Vol.1,Hadith # 54 uk.254,The book of Salat,To pray in a Church,or in a Temple etc)
Leo hii,
tumegawanyika tumegombana, ila ni kwa sababu ya Ibilisi la sivyo tungeendelea
na umoja wetu. Maana sote tunatoka kwa Baba mmoja ambapo Imani zetu
zimejengeka. Naam ndiye Ibrahim na ndiyo maana hata Mtume Muhammad na Maswahaba
wake walitambua umoja huu wa muhimu;Mwenyezi Mungu ametoa ahadi ya agano kwa Waislamu na wakristo akijua kuwa wote ni watoto wa baba mmoja ambao ni wake na
siku moja tutarejea. (Inalillah … Wa Inalillah rajun). Na ndipo anatuasa kwa
kusema maneno haya katika Torati kitabu cha kwanza Nabii Musa akisema “Agano langu nitalifanya imara kati ya mimi na wewe…….
Kuwa agano la milele, kwamba nitakuwa Mungu kwako na kwa uzao wako baada yako .
. . .”( Mwanzo: 17:7 – 8). Kwa hiyo ndugu msomaji hapa tumegundua kuwa wakristo
na Waislamu ni watoto wa Baba mmoja Ibrahimu Wakristo ni uzao Isaka na Waislamu
Ishmail hivyo ni vema tutambuane na kuizindua njia ambayo babu yetu Ibrahimu
alipitia kwa kumfuata na kumtii Mwenyezi Mungu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni