SOKA IGIN

WE INSPIRE AND EMPOWER FOR CHRIST'S MISSION.

Jumanne, 20 Machi 2018

Mikao Nane inayokubalika katika Maombi


Ifuatayo ni mikao nane ambayo inakubalika katika maombi

     i.        UKIWA KIFUDIFUDI (PROSTRATE): “Yoshua akararua mavazi yake, akaanguka kifudifudi mbele ya sanduku la Bwana hata jioni, yeye na wazee wa Israeli; wakatia mavumbi vichwani mwao.”Joshua 7:6

    ii.        UKIWA UNATEMBEA (WALKING): “Kisha akarudi akatembea  nyumbani  huko na huko mara moja; akapanda akajinyosha  juu yake; mwili wake yule mtoto ukaanza kupata moto”2Wafalme 4:35 
  iii.        UKIWA UMESIMAMA (STANDING):Ndipo wakasimama madarajani pa Walawi . . .  wakamlilia Bwana, Mungu wao, kwa sauti kuu.”Nehemia 9:5; “Nanyi kila msimamapo  na kusali, sameheni ,mkiwa na neno juu ya mtu; ili na Baba yenu aliye mbinguni awasamehe,  ninyi makosa yenu.” Marko 11:25; “ Yule Farisayo akasimama akiomba  . . .  Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali wala hakudhubutu  hata kuinua macho yake mbinguni bali alijipiga-piga kifua akisema , Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi .” Luka 18:11,13

  iv.        UKIWA UMEINUA MIKONO JUU (WITH UPLIFTED HANDS):Akasimama mbele ya madhabahu ya BWANA, machoni pa makutano wote wa Israeli, akanyosha mikono; maana Suleimani alikuwa amefanya mimbari ya shaba . . .  na kusimamisha katikati ya ua; akasimama juu yake, akapiga magoti mbele ya mkutano wote wa Israeli, akaikunjua mikono yake kuelekea  mbinguni.” 2Nyakati 6:12-13;  Ndivyo nitakavyokubariki maadamu ni hai; Kwa jina lako nitaiinua mikono yangu.” Zaburi 63:4; 

    v.        UKIWA UMEKAA (SITTING):Ndipo akaingia Daudi mfalme, akaketi mbele za Bwana; akasema, Mimi ni nani , Ee Bwana  Mungu, na nyumba yangu ni nini , hata umenileta hapa? . . . kwa maana wewe umemjua mtumwa wako  . . . Ee Bwana hakuna mwingine kama wewe wala hakuna Mungu mwingine ila wewe . . .” 1Nyakati 17:16-20

  vi.        UKIWA UMEPIGA MAGOTI (KNEELING): “Hata ikawa, Suleimani alipokwisha kumwomba  Bwana maombi hayo, na dua  hiyo yote ,akasimama na kuondoka hapo mbele ya madhabahu ya Bwana, hapo alipokuwa amepiga magoti, na kuikunjua mikono yake  kuelekea mbinguni.”1Wafalme 8:54; “”Mwenyewe  akajitenga nao  kama kiasi cha kutupa jiwe, akapiga magoti akaombaLuka 22:41; “Petro akawatoa nje wote, akapiga magoti, akaomba, kisha akaelekea yule maiti . . . .”     Matendo 9:40

 vii.        UKIWA UMESUJUDU (BOWING): “Musa akafanya haraka akainamisha kichwa chake  hata nchi  akasujuduKutoka 34:8; “Ezra akamhimidi Bwana, Mungu Mkuu .  Nao watu wote wakaitikia, Amina, Amina, pamoja  na kuinua mikono yao ; kisha wakainama vichwa vyao, wakamsujudu Bwana . . . .” Nehemia 8:6; “Naam, Wafalme wote na wamsujudie ;Na mataifa yote wamtumikie”Zaburi 72:11

viii.        UKIWA UMELALA MACHO (SLEEPING): “Basi Hezekia akajigeuza , akaelekeza uso wake  ukutani , akamwomba  Bwana  . . . .”2Wafalme 20: 2
Katika mikao yote hakuna ambao ni bora  zaidi ya mwingine ila cha muhimu sana ni ile nia ya mwombaji au roho ya maombi ya dhati hivyo waweza ukaomba ukiwa mahali popote na kwa mkao wowote. Mwandishi Ellen G. White anakubaliana na kauli hii kwa kusema kuwa “Hakuna wakati wala mahali pasipofaa kumwomba Mungu. Hakuna kinachoweza kutuzuia tusimwinulie mioyo yetu tukiwa na roho ya maombi ya dhati. Tukiwa katika makundi ya watu mitaani, katikati ya shughuli zetu za kazi, tunaweza kupeleka dua zetu kwa Mungu, na kumwomba atupe uongozi wake, kama alivyoifanya Nehemia alipotoa ombi lake mbele ya Mfalme Artashasta. Chumba cha siri cha mawasiliano kinaweza kupatikana po pote tulipo. Mlango wa moyo wetu ungefunguliwa wazi daima, na mwaliko wetu ungepanda juu ili Yesu aje na kukaa ndani ya moyo wetu kama mgeni atokaye mbinguni.”[1]

  ix.        




[1]  Ellen G. White, Njia Salama, uk.51

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni